Idara ya Mawasiliano

Dira ya Idara ya Mawasiliano ni kuwasilisha taswira chanya ya Kanisa, utume wake, maisha na shughuli zake, pamoja na kulisaidia Kanisa kuwa shahidi thabiti wa neema ya upendo na wokovu ya Yesu Kristo. Shughuli za idara huwezesha “Waadventista Wasabato kuwasiliana na matumaini kwa kuzingatia ubora wa maisha ambao umekamilika katika Kristo.” Hivyo, Idara ya Mawasiliano ya Kanisa inatimiza wajibu katika kutangaza injili ya milele kwa ufanisi na kujenga madaraja ya matumaini.

Seth Kabialo